|
Madhumuni pekee ya Madrasatunnur Educational
Trust ni kuhudumia Jamii, na tatizo liliopo kuwa hatuapati msaada
wa aina yoyote wa kila tuitegemee jamii yenyewe yaani nikizungumza
hivi ina maana ni (wewe).
Juu ya hivyo tutazidi kumshukuru Allah pamoja
na wewe ikiwa utaweza msaada wa aina yoyote ambao umo ndani ya
uwezo wako,lakini njia bora na njema kabisa ikiwa utaweza
kutusaidia kwa kutoa msaada wa kifedha, ukihisi waweza kututsaidia
kwa njia nyengine zaidi ya hiyo basi tafadhali tunakuomba wasiliana
nasi kwa kutuandikia email kwenye anuani hii
hapa
Sehemu nyengine ya kusomeshea
Kwa muda mrefu sasa tumekuwa tukipata tabu
katika sehemu ya kusomeshea vijana hadi watu wazima pale wanapokuja
kutafuta elimu, sehemu tuliokodi inagharimu fedha nyingi na kama
tulivyosema kuwa mara zote huwa tunategemea Sadaqah kutoka kwa
jamii ili kuendeleza taasisi hii, na mchango mkubwa hutolewa na
wazee wa wanafunzi. Kwa sasa kila mwaka tunalipa jumla ya £7000.
kwa mwaka, na fedha hizo ni kwa ajali ya siku za Jumamosi na
Jumapili tu kwa wiki, ni Jumla ya masaa 9, kwa siku zote mbili.
(Jumamosi masaa 5 na Jumapili Masaa 4)
Kutokana na maombi mengi ya wazazi ya kutaka
watoto wao kuja kupata elimu hapa kwenye madrasah, tunashindwa
kuwapokea kutokana na sehemu tuliyokodi ni ndogo vile vile, kwa
mujibu wa taratibu za afya na usalama ukumbi tulionao umeruhusiwa
kuchukua watu wasiozidi 90, lakini hadi sasa tuna wanafunzi
wasiopungua 176.
Ili tuweze kupata sehemu nyengine iliokuwa kubwa na iwe ya mali yetu kama Jamii, tumeanzisha mfuko maalumu kwa ajili ya maradi huu ambao umeanza mwezi wa October 2009. Na tayari tumeshaanza kupokea michango kutoka kwa watu mbali mbali.
Shabaha yetu ni kukusanya jumla ya £700.000.00. Na Ishaallah tutafanikiwa na tunakuomba nawe pia ujiunge pamoja nasi kwenye jambo hili la kheri. na ukurasa huu utakuwa ukiwajuulisha Ummah jumla ya mapato yaliopatikana kila mwezi Inshaallah. (Hadi mwisho wa Mwezi wa October tumeshakusanya £1170.00)
TUNAHITAJI MSAADA WAKO SASA
Unaweza kufanya malipo moja kwa moja kwenye Account ya Madrasah
| Islamic Bank of Britain |
| Madrasatunnur Educational Trust |
| A/C No: 01158850 |
| S/C No: 30-00-83 |
Ama waweza kutoa mchango wako kwa kutumia PAYPAL
Vile vile tunakuomba kama wewe ni mkaazi wa UK na mlipa kodi (Tax), Tafadhali tunakuomba Dowload fomu unayoitwa Gift Aid, ijaze fomu hiyo kisha turejeshee.kwani fomu hiyo ukijaza itawezekana kupata ongezeko la asimilia 28% ya mchango wako kutoka Inland Revenue
Download:
Gift Aid Form &
Standing order mandate
|